Kumbukumbu la Blogu

Jumatatu, 23 Septemba 2019

SIRI 5 KUBWA ZA MAFANIKIO

Kila binadamu ameumbwa na kiu ya kufanikiwa katika kila kitu anachofanya. Mafanikio ndio kilele cha mlima mkubwa wa maisha ambao umejengwa kwa misingi na ngazi za mihangaiko na mitihani ambayo unapaswa kuivuka ili upumzike kwenye kilele hicho.

Kwa bahati mbaya, unaposema ‘mafanikio’ wengi hufikiria kuhusu ‘utajiri’. Lakini ukweli ni kuwa kuna tofauti kati ya kuwa tajiri na kufanikiwa kiuchumi. Unaweza kuwa tajiri lakini ukawa bado hujafanikiwa. Kwa kuwa watu wanawaza utajiri kuwa ndio kigezo cha mafanikio hujikuta wakijiingiza kwenye vitendo vya ajabu kwa lengo la kujizolea mali lakini mwisho huwa wanagundua kuwa hawajafanikiwa japo jamii inahisi wamefanikiwa.

Nanachoamini mimi, kufanikiwa kweli ni kutimiza malengo yako kwa ufanisi na kwa wakati, lakini mafanikio hayo yakupe amani moyoni mwako (peace of mind).

Vinginevyo, utafanikiwa kwa mrundikano wa fedha huku ukitengeneza tatizo kubwa zaidi la msongo wa mawazo na ukosefu wa amani ya moyo. Hivyo, mafanikio ya njia ya mkato ni mafanikio feki yanayokuja na matatizo mengi mazito zaidi.

Kwa utangulizi huo mrefu, naamini utanielewa zaidi napokupitisha kwenye hizi ‘siri za wazi’ za mafanikio ya kweli katika maisha.

1. Jiamini

Mafanikio ya kweli yanaanza na wewe. Hivyo, kujiamini ni msingi mzuri utakaokufanya utambue uwezo wako katika kufanya jambo fulani. Amini uwezo wa kufanya jambo hilo uko mikononi mwako. Usijishushe, jipime kwa mengi mazuri unayoweza kufanya, ikatae roho ya kujiona huwezi.

2. Thubutu

Neno hili pia ni msingi wa pili mkuu wa mafanikio. Uoga wa kuthubutu ni kikwazo kikuu kinachowarudisha wengi nyuma na kujikuta hata kuanza safari ya mafanikio hawawezi. Jambo lolote zuri na kubwa huwa gumu kufanya na ni rahisi kuhisi haliwezekani. Usikubali kushindwa bila kujaribu. Thubutu kwa dhati na weka nguvu yako na akili yako yote katika uthubutu huo. Hata hivyo, katika uthubutu huu, unapaswa kupima vizuri ili uchukue ‘calculated risk’ na sio ‘just risk

3. Panga na tekeleza kwa vitendo

Kumbuka, ukishindwa kupanga ujue umepanga kushindwa. Kuwa na mipango inayopimika na kutekelezeka kwa kiwango cha juu. Usiwe na mipango tu mikubwa ambayo hata utekelezaji wake hauwezekani. Unapopanga fikiria wapi utapata rasilimali na jinsi ya kutelezeka, lakini pia mpango wako ukupe uwezo wa kuutathmini na kujipima mwisho wa kazi hiyo. Hata hivyo, mipango haitakuwa na maana kama hautaitekeleza kwa ufanisi. Ukishindwa kutekeleza mpango wako, rudi angalia ulipoteleza ili urekebishe na sio kuufuta mpango mzima bila sababu za msingi.

4. Tengeneza mtandao na wasiliana

Mtandao ni kama daraja au miundombinu ya kuyafikia mafanikio. Hakikisha haujifungii kwenye dunia yako peke yako. Hakikisha kila unaekutana naye na kupata nafasi ya kumfahamu kama mtu anayeweza kuwa sehemu ya daraja bora kwa namna moja au nyingine, anakuwa sehemu ya mtandao wako.

Lakini kuwa na mtandao wa watu pekee hautoshi kama hautawasiliana nao. Kuwasiliana na mtandao huo ni kuufanya uwe ‘active’ ili isionekane kama unawatafuta wakati ukiwa na shida tu. Aidha, unapaswa kujipima kwa kuangalia watu wangapi wanakufahamu wewe zaidi ya watu wangapi unaowafahamu. Kwa mfano: wewe unamfahamu Mkurugenzi wa kampuni ‘A’, Jiulize, je, yeye anakufahamu? Kama hakufahamu basi yeye sio sehemu ya mtandao wako.

Lakini pia, angalia mawasiliano yako ya siku, wangapi umeongea nao kuhusu wazo la biashara au kazi.

5. Kuwa mkweli na Mwaminifu

Hii ni siri kubwa zaidi ya zote, japokuwa nimeiweka mwishoni kati ya hizi tano. Usipokuwa mwaminifu na mkweli huku unaona mambo yako yanaenda vizuri unapaswa kushtuka mapema. Wewe ni kama mtu anaevuka ng’ambo ya pili huku akilivunja daraja. Mwisho wa siku utajikuta unaporomoka kabla hujafika unakotakiwa kufika.

Uaminifu utaimarisha mtandao wako kwa hali ya juu zaidi na utatafutwa kwa kuwa wewe utakuwa sehemu ya sababu ya mafanikio ya watu wengine. Kwa mfano, angalia namba ulizonazo kwenye simu yako ya mkononi. Je, ukitaka kumpigia simu dereva taxi majira usiku au hata muda wa kawaida utatumia vigezo gani? Bila shaka uaminifu na ukweli vitatangulia zaidi.

Kuwa mwaminifu na mkweli kwa kila mtu utakayefanya nae kazi, biashara au hata wakati mnafanya mambo ya kawaida ya kijamii kunakupa nafasi ya kuwa chaguo la kwanza kwa watu wanapohitaji huduma, bidhaa au rasilimali ambayo unayo.

Ukifuata kwa uhakika haya matano huku ukimkumbuka Mungu wako kwa kila jambo utafanikiwa kweli na kubaki na amani ya moyo.

JIFUNZE KUSAMEHE

Wewe na mwenzi wako mnapogombana, mnataja tena orodha ya makosa ya wakati uliopita, mnakumbushana mambo mabaya mliyotendeana zamani ambayo yalipaswa kusuluhishwa muda mrefu uliopita. Tatizo ni nini? Huenda mmoja wenu au nyote wawili hamjui jinsi ya kusamehe.


Mnaweza kujifunza kusameheana. Hata hivyo, kwanza, fikiria kwa nini huenda mume na mke wakaona ni vigumu kusameheana.

KWA NINI HILI HUTOKEA?

Mamlaka. Waume na wake fulani huamua kutosamehe ili wawe na kiasi fulani cha mamlaka juu ya wenzi wao. Halafu, wanapogombana, wanatumia matukio ya wakati uliopita kuwadhibiti wenzi wao.

Kinyongo. Mtu anapokosewa anaweza kuendelea kukumbuka jambo hilo kwa muda mrefu. Huenda mwenzi wa ndoa akasema ‘nimekusamehe’ lakini bado afungie kinyongo—na labda hata apange kulipiza kisasi.

Kukatishwa tamaa. Watu fulani huingia katika ndoa wakiamini kabisa kwamba maisha yao yatakuwa ya raha mustarehe. Kwa hiyo, kutoelewana kunapotokea, wanajiuliza inawezekanaje kwamba mwenzi waliyefikiri anawafaa kabisa ana maoni tofauti na yao. Matarajio yasiyo halisi yanaweza kumfanya mtu awe na kawaida ya kutafuta makosa na asiwe tayari kusamehe.

Kutoelewa kusudi la kusamehe. Watu wengi hukataa kuwasamehe wenzi wao kwa sababu hawaelewi kusudi la kusamehe. Kwa mfano, wao hujiambia:

Nikimsamehe, nitakuwa nikipunguza uzito wa kosa.

Nikimsamehe, lazima nisahau alichotenda.

Nikimsamehe, atanitendea vibaya hata zaidi.

Kwa kweli, kusamehe hakumaanishi mambo yatakuwa kama yalivyotajwa hapo juu. Hata hivyo, bado inaweza kuwa vigumu kusamehe—hasa kwa watu wenye uhusiano wa karibu kama mke na mume.

 MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Fahamu maana ya kusamehe. Katika Biblia, nyakati nyingine neno “samehe” linamaanisha “kuachilia.” Kwa hiyo, kusamehe hakumaanishi kwamba mara zote unapaswa kusahau mambo yaliyotokea au kupunguza uzito wa kosa. Nyakati nyingine kunaweza kumaanisha kuachilia mambo kwa manufaa yako na ya ndoa yako.

Tambua matokeo ya kutosamehe. Wataalamu fulani wanasema kwamba kuweka kinyongo kunaweza kusababisha matatizo ya kimwili na kihisia, yanayotia ndani kushuka moyo na kupanda kwa shinikizo la damu—isitoshe kunaweza kuharibu ndoa yako. Biblia ina sababu nzuri inaposema hivi: “Iweni wenye fadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyororo, mkisameheana kwa hiari.”—Waefeso 4:32.

Tambua faida za kusamehe. Roho ya kusamehe inawasaidia watu waliofunga ndoa waamini kwamba mwenzi wao hakuwa na nia mbaya alipowakosea na hivyo kuepuka kuhesabu mabaya. Kufanya hivyo kutawasaidia kujenga mazingira yanayozuia chuki na kuruhusu upendo kukua.—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 3:13.

Ona mambo kihalisi. Ni rahisi zaidi kusamehe ikiwa unamkubali mwenzi wako jinsi alivyo, licha ya upungufu wake. Kitabu Fighting for Your Marriage (Jinsi ya Kuiokoa Ndoa Yako) kinasema kwamba unapokazia fikira udhaifu wa mwenzi wako huenda ukasahau sifa zake nzuri. Kitabu hicho kinauliza hivi: “Ni nini hasa ambacho ungependa kukazia fikira kwa kuwa tayari umefunga ndoa?” Kumbuka, hakuna mtu mkamilifu—kutia ndani wewe.—Kanuni ya Biblia: Yakobo 3:2.

Uwe mwenye kukubali sababu. Wakati ujao unapokasirishwa na jambo fulani ambalo mwenzi wako amesema au kufanya, jiulize hivi: ‘Je, kweli jambo hilo ni muhimu? Je, lazima niombwe msamaha, au naweza kupuuza kilichotokea na kusonga mbele?’—Kanuni ya Biblia: 1 Petro 4:8.

Ikiwa ni lazima, zungumzieni jambo hilo. Eleza kwa utulivu jambo lililokukasirisha, na kwa nini unahisi hivyo. Usishuku kwamba mwenzi wako ana nia mbaya na usishikilie sana maoni yako, kwa kuwa kufanya hivyo kutamfanya tu mwenzi wako ajitetee. Badala yake, eleza tu jinsi matendo ya mwenzi wako yalivyokuathiri.

JIFUNZE KUSAMEHE

Wewe na mwenzi wako mnapogombana, mnataja tena orodha ya makosa ya wakati uliopita, mnakumbushana mambo mabaya mliyotendeana zamani ambayo yalipaswa kusuluhishwa muda mrefu uliopita. Tatizo ni nini? Huenda mmoja wenu au nyote wawili hamjui jinsi ya kusamehe.


Mnaweza kujifunza kusameheana. Hata hivyo, kwanza, fikiria kwa nini huenda mume na mke wakaona ni vigumu kusameheana.

KWA NINI HILI HUTOKEA?

Mamlaka. Waume na wake fulani huamua kutosamehe ili wawe na kiasi fulani cha mamlaka juu ya wenzi wao. Halafu, wanapogombana, wanatumia matukio ya wakati uliopita kuwadhibiti wenzi wao.

Kinyongo. Mtu anapokosewa anaweza kuendelea kukumbuka jambo hilo kwa muda mrefu. Huenda mwenzi wa ndoa akasema ‘nimekusamehe’ lakini bado afungie kinyongo—na labda hata apange kulipiza kisasi.

Kukatishwa tamaa. Watu fulani huingia katika ndoa wakiamini kabisa kwamba maisha yao yatakuwa ya raha mustarehe. Kwa hiyo, kutoelewana kunapotokea, wanajiuliza inawezekanaje kwamba mwenzi waliyefikiri anawafaa kabisa ana maoni tofauti na yao. Matarajio yasiyo halisi yanaweza kumfanya mtu awe na kawaida ya kutafuta makosa na asiwe tayari kusamehe.

Kutoelewa kusudi la kusamehe. Watu wengi hukataa kuwasamehe wenzi wao kwa sababu hawaelewi kusudi la kusamehe. Kwa mfano, wao hujiambia:

Nikimsamehe, nitakuwa nikipunguza uzito wa kosa.

Nikimsamehe, lazima nisahau alichotenda.

Nikimsamehe, atanitendea vibaya hata zaidi.

Kwa kweli, kusamehe hakumaanishi mambo yatakuwa kama yalivyotajwa hapo juu. Hata hivyo, bado inaweza kuwa vigumu kusamehe—hasa kwa watu wenye uhusiano wa karibu kama mke na mume.

 MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Fahamu maana ya kusamehe. Katika Biblia, nyakati nyingine neno “samehe” linamaanisha “kuachilia.” Kwa hiyo, kusamehe hakumaanishi kwamba mara zote unapaswa kusahau mambo yaliyotokea au kupunguza uzito wa kosa. Nyakati nyingine kunaweza kumaanisha kuachilia mambo kwa manufaa yako na ya ndoa yako.

Tambua matokeo ya kutosamehe. Wataalamu fulani wanasema kwamba kuweka kinyongo kunaweza kusababisha matatizo ya kimwili na kihisia, yanayotia ndani kushuka moyo na kupanda kwa shinikizo la damu—isitoshe kunaweza kuharibu ndoa yako. Biblia ina sababu nzuri inaposema hivi: “Iweni wenye fadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyororo, mkisameheana kwa hiari.”—Waefeso 4:32.

Tambua faida za kusamehe. Roho ya kusamehe inawasaidia watu waliofunga ndoa waamini kwamba mwenzi wao hakuwa na nia mbaya alipowakosea na hivyo kuepuka kuhesabu mabaya. Kufanya hivyo kutawasaidia kujenga mazingira yanayozuia chuki na kuruhusu upendo kukua.—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 3:13.

Ona mambo kihalisi. Ni rahisi zaidi kusamehe ikiwa unamkubali mwenzi wako jinsi alivyo, licha ya upungufu wake. Kitabu Fighting for Your Marriage (Jinsi ya Kuiokoa Ndoa Yako) kinasema kwamba unapokazia fikira udhaifu wa mwenzi wako huenda ukasahau sifa zake nzuri. Kitabu hicho kinauliza hivi: “Ni nini hasa ambacho ungependa kukazia fikira kwa kuwa tayari umefunga ndoa?” Kumbuka, hakuna mtu mkamilifu—kutia ndani wewe.—Kanuni ya Biblia: Yakobo 3:2.

Uwe mwenye kukubali sababu. Wakati ujao unapokasirishwa na jambo fulani ambalo mwenzi wako amesema au kufanya, jiulize hivi: ‘Je, kweli jambo hilo ni muhimu? Je, lazima niombwe msamaha, au naweza kupuuza kilichotokea na kusonga mbele?’—Kanuni ya Biblia: 1 Petro 4:8.

Ikiwa ni lazima, zungumzieni jambo hilo. Eleza kwa utulivu jambo lililokukasirisha, na kwa nini unahisi hivyo. Usishuku kwamba mwenzi wako ana nia mbaya na usishikilie sana maoni yako, kwa kuwa kufanya hivyo kutamfanya tu mwenzi wako ajitetee. Badala yake, eleza tu jinsi matendo ya mwenzi wako yalivyokuathiri.

TATIZO SIO MTAJI NI WEWE TU

Hawa ni wale wenye shauku kubwa moyoni mwao kufanya jambo la pekee na hawafanyi lakini ukiwauliza watakupangia sababu nyingi za kuhalalisha ...